Join   AY.CO.TZ   

»   Ay » Highlights 

A.Y Kufanya Kazi na P-Square  


A.Y Kufanya Kazi na P-Square

Kutokana na muziki wa bongo flava kufanikiwa kupenya katika mipaka ya nchi za Afrika ya Mashariki; ambapo katika nchi kama Kenya,Uganda,Burundi na Rwanda muziki huo umetokea kupendwa mpaka kufunika mpaka nyimbo zingine za nchi hizo;sasa zinaonekana dalili za muziki huo kwenda mbali zaidi.

Msanii mmoja wapo ambae anahusika kuutangaza muziki huo ndani na nje ya nchi Ambwene Yessayah “A.Y” ameamua kuuchukua muziki huo na kuupeleka Afrika Magharibi kwa ajili ya kuutangaza zaidi.
 
 

Video Mpya ya Mwana FA na A.Y Wiki Hii  




Baada ya kufunika vilivyo katika Sauti za Busara Visiwani Zanzibar nyota wa bongo flava Mwana FA na A.Y wanatarajia kutoa video mpya wa wimbo unaoitwa “NANGOJA AGEUKE” .Wimbo huo ambao unapatikana katika album yao ambayo ipo mtaani inayoitwa “HABARI NDIO HIYO”.Wimbo huo uliotengenezwa na producer mkali “Hermy B” ambaye pia alitengeneza wimbo mwingine uitwao Habari ndio hiyo unaosumbua anga la muziki wa Afrika Mashariki .

“Video ya wimbo huo imefanyika hapa hapa Dar es Salaam na kampuni ya Ogopa Dj’s kutoka Kenya,video ni kali sana na tunategemea watu wataifurahia na kuburudika nayo…itatoka ijumaa hii kwa hiyo watu wakae karibu na runinga zao..”alikaririwa Mwana fa.

Picha za shooting ya video hiyo na za Sauti za Busara tutawawekea mapema iwezekanavyo.
 
 

A.Y Afungua Unity Entertainment  


A.Y Afungua Unity Entertainment

Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Ambwene Yessayah (A.Y),anatarajia kufungua kampuni yake unayohusiana na burudani.Akifanya mahojiano kupitia mtandao huu..

Mwandishi: Mambo vp mzee wa commercial?
A.Y: Poa!

Mwandishi: A.Y mimi nilikuwa na mambo kadhaa ya kuongea na wewe kuhusiana na biashara yako ya kimuziki zaidi.
A.Y: Hakuna tatizo kaka endelea…tu

Mwandishi: A.Y upo kwenye hii fani muda mrefu sana na kusema ukweli kabisa wewe sasa ni mmoja kati ya wasanii waliochangia kuinua muziki huu,kuna tetesi kuwa una mpango wa kufungua kampuni?
A.Y: Ni kweli kabisa,na sasa ipo katika hatua za mwisho mwisho mwezi wa pili tarehe moja kazi itaanza rasmi namshukuru Mungu mambo yote yanaenda sawa.
 
 

Funga na Fungua Mwaka Ilivyofunika  


Msanii wa bongo flava nchini A.Y au ukipenda mzee wa commercial alifanya burudani kali katika maonyesho tofauti yaliyofanyika mwezi desemba katika kumbi za Malaika House-Dar es Salaam tarehe 21, Tripple A-Arusha tarehe 25 siku ya krismasi,uwanja wa CCM Kirumba-Mwanza tarehe 29 na tarehe 31 mkesha wa mwaka mpya Ngome Kongwe mjini Zanzibar ambapo yalikuwa maonyesho rasmi kwa mshindi wa Big Brother Africa 2007 Richard Bezuidenhout kuwashukuru watanzania wenzake kwa kumfanya aibuke mshindi katika shindano la Big Brother Africa 2. Katika show hizo AY alikuwa sambamba na wasanii wenzake kama Juma Nature na mkali anayetesa na nyimbo yake “Hapo Vipi” katika chart mbalimbali za bongo Prof.Jay.Wote waliweza kumsindikiza vema mshindi huyo wa jumba la BBA 2007.
 
 

Makamuzi ya Nguvu Leo Ndani ya Nairobi  


Makamuzi ya Nguvu Leo Ndani ya Nairobi

Leo tarehe 11 December kuanzia saa tatu usiku A.Y atakuwepo katika viwanja vya Carnival Jijini Nairobi katika uzinduzi wa album mbili za wanamuziki maarufu wa Kenya Amani na Nonini.

Mzee wa Commercial ambaye tangu kipindi cha nyuma mpaka sasa amezidi kufanya vizuri na kujizolea washabiki wengi zaidi nchini humo amepata mualiko huo maalum ambao unaambatana na mkesha wa siku ya Uhuru wa Kenya.

Makamuzi yaliyoandaliwa na A.Y kwa ajili ya usiku wa leo ni makubwa sana na kilichobakia ni kusubiri muda wa tukio.

Kama kawaida yetu tutawaletea habari na picha za yaliyojiri usiku wa leo.
 
 

"Usiku wa Undani Wangu" Wafunika  


"Usiku wa Undani Wangu" WafunikaUsiku wa Ijumaa tarehe 16 November jijini Dar es Salaam kulifanyika tukio moja la kihistoria katika muziki wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla ambapo mwanamuziki Ambwene Yessayah a.k.a A.Y aliweza kuzindua kwa mafanikio tovuti yake binafsi iitwayo www.ay.co.tz ,documentary yake inayoenda kwa jina la “Undani Wangu” pamoja na nguo zake zinazotambulika kama “Commercial Wear”.

Umati mkubwa uliweza kujitokeza kwenye ukumbi wa maraha wa Club Maisha ulioko Oysterbay.Uzinduzi huo iliofana ulidhaminiwa na Str8 Muzik na kutayarishwa na Lips Entertainment uliweza kuwavutia washabiki wengi sana ambao walionyesha utulivu wa hali ya juu hali ambayo iliashiria kuwa ni jinsi gain wanaridhika na mpangilio mzima wa tukio zima la siku hiyo.
 
 

Sasa ni Coco Baech  


Siku ya Jumapili tarehe 9 mwezi huu wa kumi na mbili pale COCO BEACH Mzee wa Commercial A.Y ataungana na wasanii wenzake wa Bongo Flava na kukamua sana katika tamasha la bure lililoandaliwa na kinywaji bora kinachopendwa sana na vijana kitambulikacho kwa jina la FANTA.

A.Y ambae wiki iliyopita aliweza kufanya vizuri sana katika matamasha tofauti yaliyofanyika Arusha na Mwanza ambapo kulijumuishwa na wasanii tofauti toka Afrika ya Mashariki;
 
 

Usiku wa Undani Wangu  


Usiku wa Undani Wangu
Uzinduzi wa: - Documentary “UNDANI WANGU” -Clothing line “Commercial Wear”

Uzinduzi wa: - Documentary “UNDANI WANGU” -Clothing line “Commercial Wear”

Wasanii wakali kutoka Afrika Mashariki watamsindikiza A.Y kwa kutoa burudani kali ni…

-Juacali (Kenya) -Michael Ross (Uganda) -Juma Nature (Tanzania) na -Besta (Tanzania)

VENUE; CLUB MAISHA

DATE: 16th November 2007

ENTRANCE: 7000 TU.

SHOW HII IMEDHAMINIWA NA STRAIGHT MUZIK-SM
 
 

A.Y na Prezzo Wazua Balaa Nairobi  


A.Y na Prezzo Wazua Balaa Nairobi

AY, Athur and Prezzo

Ambwene Yessayah ambae washabiki wa muziki wanamfahamu kama A.Y-mzee wa commercial,wiki ya jana aliweza kufanya umati wa watu kubaki midomo wazi kwa kumpigia mayowe baada ya kuibuka ghafla “kisapraizi” bila washabiki kujua kama alikuwa maeneo hayo viwanja vya Carnivore jijini Nairobi-Kenya.
 
 

A.Y Kuzindua Tatu Pamoja!  


A.Y Kuzindua Tatu Pamoja!Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini A.Y tarehe 16 mwezi November anatarajia kufanya uzinduzi wa iliyo katika mfumo wa video inayoelezea historia ya maisha yake ya kimuziki na maisha yake binafsi (Documentary).

Ndani yake kutakuwa na maoni ya wadau tofauti,wanamuziki wenzake,madj’s,watangazaji,familia yake pamoja na washabiki kwa ujumla,shows zake na video zake zote tangu alipokuwa na miaka kumi na moja mpaka mpya mpaka ambazo hazijatoka bado.