Join   AY.CO.TZ   

»   Ay » Highlights » Funga na Fungua Mwaka Ilivyofunika 

Funga na Fungua Mwaka Ilivyofunika


Msanii wa bongo flava nchini A.Y au ukipenda mzee wa commercial alifanya burudani kali katika maonyesho tofauti yaliyofanyika mwezi desemba katika kumbi za Malaika House-Dar es Salaam tarehe 21, Tripple A-Arusha tarehe 25 siku ya krismasi,uwanja wa CCM Kirumba-Mwanza tarehe 29 na tarehe 31 mkesha wa mwaka mpya Ngome Kongwe mjini Zanzibar ambapo yalikuwa maonyesho rasmi kwa mshindi wa Big Brother Africa 2007 Richard Bezuidenhout kuwashukuru watanzania wenzake kwa kumfanya aibuke mshindi katika shindano la Big Brother Africa 2. Katika show hizo AY alikuwa sambamba na wasanii wenzake kama Juma Nature na mkali anayetesa na nyimbo yake “Hapo Vipi” katika chart mbalimbali za bongo Prof.Jay.Wote waliweza kumsindikiza vema mshindi huyo wa jumba la BBA 2007.

Mtandao huu ulipata fursa ya kuongea na kila mtu A.Y alisema…wakazi wa sehemu zote walizopita walijitokeza kwa wingi kumpokea kwa shangwe na furaha kubwa mshindi wa jumba hilo la BBA kwani kitendo cha kushinda na kupita kuwashukuru watanzania wenzake kimewapa faraja kubwa kwao. Prof Jay pia naye alinasawa na mtandao huu akisema “hii ni kama karama Richard aliyepewa na mwenyezi Mungu,kwani ni washiriki wengi walioshiriki katika nchi tofauti,lakini katika hizo nchi wengi wao waliweza kumpigia kura mshiriki aliyewakilisha Tanzania na kuibuka kifua mbele na kuweza kupeperusha bendera yetu vema.Mimi kama heavy weigth mc wengi huniita hivyo nimefurahia sana kuona mambo yalivyokwenda vizuri hata wasanii tuliyokuwepo katika tour hii ya nikimaanisha mimi,Juma Nature na A.Y tulisababisha burudani kali kabisa,zile silaha(nyimbo) za zamani na mpya ziliwakilishwa vyema..alimalizia kwa kusema mtu mbili kama elfu mbili”.

Sir Nature na alipata fursa ya kuongea na mtandao huu alisema alifurahishwa sana na ziara hiyo na anaamini mwaka 2008 ni mwaka wa kazi na washabiki wasubiri mambo makubwa kutoka kwake.Pia mtandao huu uliweza kumshika Richard katika mgahawa wa Sub Way pale maeneo ya Shoppers Plaza Msasani akiwa ameongozana na mshirki mwenzake Code kutoka Malawi;

Richard alisema kwanza kabisa anamshukuru Mwenyezi Mungu,wazazi,mkewe Ricky,multi choice Tanzania,Bia ya Serengeti,Red Promotion na zaidi ziwaendee watanzania kwa pamoja wote walioweza kumpigia kura na hata wale wasioweza kwani kwa imani zao waliweza kumuombea kwa Mungu na kuibuka kidedea katika jumba la Big Brother Africa 2007.

Maonyesho mengine ya A.Y aliyoweza kuyafanya vizuri pia ni kama la Coco Beach tarehe 30 Desemba na onyesho lingine lililobeba watu wengi sana lililofanyika Korogwe-Tanga kwenye ukumbi wa Mamba Club.
  Discuss
Hello Guest. Please register or login to view hidden text..
Related News
  • Sasa ni Coco Baech
  • Tour ya A.Y Kenya Yafunika
  • Tour Nyingine ya A.Y Inakaribia Kuanza
  • A.Y Ndani ya Dubai
  • A.Y Kumuunga Mkono Mh. Rais J.K Kikwete
  • Share

    #2 Author: barker 7 December 2011 12:39


    Kevin Wilson
    canada

    Great gifts: You can also buy REPica DEsigner Handbags to gift them to your friends and loved ones without spending too much. They are just a perfect gift for any occasion whether it’s a birthday, anniversary, or any other special day. Replica designer bags will surely bring a smile on your loved ones face especially if they are a fashion freak.

        
    Members of Guest cannot leave comments.