A.Y ambae wiki iliyopita aliweza kufanya vizuri sana katika matamasha tofauti yaliyofanyika Arusha na Mwanza ambapo kulijumuishwa na wasanii tofauti toka Afrika ya Mashariki;
Tulipata fursa ya kupata maelezo toka kwake jinsi mambo yalivyojiri huko alikotoka na amejiandaaje na matamasha ya siku zijazo….
“Arusha tulikuwa na show tarehe 30 Novemba ya East Africans Finest katika viwanja vya Tripple A ambapo niliweza kuwa jukwaa moja na Prof Jay,Redsan,Mwana Fa,Lady JD,Nako 2 Nako,Michael Ross,Nonini,Juacali na T.I.D.Nafurahi na kupata moyo sana kwa kuona jinsi kazi zetu zinavyokubalika.Pia nikaenda Mwanza Ccm Kirumba katika tamasha la Siku ya Ukimwi duniani.siku hii huwa inaadhimishwa kila mwaka tarehe 1 mwezi wa kumi na mbili.Imenipa moyo sana kwa vile vijana wengi sana wa Mwanza waliweza kujitokeza na kuitikia wito.Huko pia nilikuwa na Mwana Fa,Fid Q,H Baba,Flora Mbasha pamoja na Hard Mad”.
“Sasa ni Coco Beach tarehe 9 moto ule ule.Tujitokeze kwa wingi tufurahie kwa pamoja Habari ndio hiyo.Alimalizia kwa kusema hivyo…


