Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini A.Y tarehe 16 mwezi November anatarajia kufanya uzinduzi wa iliyo katika mfumo wa video inayoelezea historia ya maisha yake ya kimuziki na maisha yake binafsi (Documentary).Ndani yake kutakuwa na maoni ya wadau tofauti,wanamuziki wenzake,madj’s,watangazaji,familia yake pamoja na washabiki kwa ujumla,shows zake na video zake zote tangu alipokuwa na miaka kumi na moja mpaka mpya mpaka ambazo hazijatoka bado. Album hiyo ikiwa imepewa jina la “UNDANI WANGU” ikiwa kazi nzima ya uchukuaji picha imesimamiwa na Tripod Media wakishirikiana na 2Eyez Production inatarajia kuingia mtaani mwanzoni mwa mwezi ujao.
A.Y alisema kupitia mtandao wake “mashabiki wangu watarajie vitu vikubwa zaidi ya hivi karibuni na tofauti kutoka kwangu,kwani hivi sasa nipo mbioni na maandalizi ya kuzindua documentary yangu”.Vilevile hakuishia hapo alisema ya kwamba “siku hiyo siyo documentary tu itakayozinduliwa bali pia website yangu ya www.ay.co.tz ambayo inamrahisishia kazi ya kujitangaza pande zote duniani,mavazi ya kike na kiume yatayokuwa na jina lake ambazo yametengenezwa kwenye ubora wa juu kabisa”.
A.Y akiendelea kulonga kupitia mtandao wake alisema lengo ni kukuza muziki wake na kuzidisha changamoto kwenye muzki kiujumla na kuwafanya washabiki wake wamuelewe kiundani zaidi.
A.Y anatarajia kutangaza ukumbi utaofanyika tukio hilo la kihistoria na wasanii wataomsindikiza usiku huo ambao wanatamba afrika mashariki siku chache zijazo kupitia vyombo vyote vya habari..


