Msanii wa muziki wa bongo flava nchini ambaye kwa sasa yupo juu ile mbaya na single yake kali ya USIJARIBU A.Y,anatarajia kufanya maonyesho MANNE kabambe katika mikoa mitatu tofauti.Ambapo show ya kwanza itaanza mkoani Dodoma JUMAMOSI tarehe 14 April 2007 ndani ya NK DISCO halafu moto utaendelea kuwashwa kesho yake jumapili tarehe 15 April 2007 ndani ya ukumbi wa KILIMANI,ambayo itakuwa ni ya kutafuta vipaji vitakavyo shiriki katika TUZO ZA KILIMANJARO - 2007.Show ya tatu itakuwa Mkoani Mbeya JUMAMOSI tarehe 21 April ndani ya ukumbi wa DANDHOO HALL nayo pia ni show ya kutafuta vipaji vitakavyoshiriki katika TUZO KUBWA ZA KILIMANJARO 2007,kisha baada ya hapo MZEE WA COMMERCIAL atadondoka ndani ya Morogoro na atatoa burudani kwa wakazi wa mji kasoro bahari na maeneo ya jirani yanayozunguka mkoa huo ndani Ukumbi wa BWALO LA UMWEMA.Show hiyo ikiwa imeandaliwa na RAM"S ENTERTAIMENT.
-WAKAZI WOTE AMKAE TAYARI KUPATA SHOW KALI- KUTOKA KWA AY....


