Lyrics
    Binadamu
    Intro: This is A.Y from Tanzania, Maurice Kirya and Hamdee from Uganda.
    It’s a dedication to all African who living in poverty.

    Verse I.
    Usiombee mambo yaharibike.
    Pesa usiishike, mfano wa mti upukutike.
    Utaonekana si lolote si chochote.
    Utaonekana karaha kwa watu siku zote.
    Walimwengu hawatakupa  mikono.
    Magonjwa yatakuvuta ndani ya shimo.
    Utakata tamaa, utaandama na balaa.
    Pumzi hutovuta kwa raha, kweli usiombee kuwahi.
    Survive for fittest; never trust nobody in this world of weakness
    Watakukana hata kama ndugu zako.
    Watadiriki sema hawajui hutokako
    Mama acha kulia, Hayo uliyonayo ni majaribu tu ya dunia. Ipo siku mambo yako yatatulia.
    Utasahau hata Mabaya ya zamani uliyopitia ooh hii dunia…

    Chorus.
    Bagalalinaa, Gendo kole,
    You should think about tomorrow
    Not only today
    Bagalalinaa, Gendokolee
    Uuh, Gendokoleee
    Yeeeh

    Verse II.
    Wapo wapi marafiki uliokuwa nao
    Enzi zile pesa imekutembelea
    Wako wapi sasa? Hawapo wamekukimbia
    Sasa huko waliko tayari wanakukandia.
    Ada ya watoto hujalipia, kodi ya chumba nayo unadaiwa,
    unazidi changanyikiwa. Hata unajuta oh kwanini ulizaliwa.
    Piga moyo konde, Maisha uyashinde.
    Bado safari ndefu yenye miba na mabonde
    Usiweke kinyongo hata kama walikutupa
    Remain strong in this world.
    Don’t be jealous, Dat’s all…

    Chorus.
    Bagalalinaa, Gendo kole,
    You should think about tomorrow
    Not only today
    Bagalalinaa, Gendokolee
    Uuh, Gendokoleee
    Yeeeh

    Bridge
    Binadamu sio watu.
    Ukiwa na shida hutowaona.
    Ona sasa wamekimbia.
    Ona sasa wamekimbia.

    Chorus.

    Written by: - Ambwene Yessaya, Hamdee Kiwamba & Maurice kirya

    Produced by: - Henry from No End Production.
    Mixed by: - Master Jay from MJ Production
    Video by: - Paparazzi.


Lyrics
    Yule

    Intro: (Aha) (Aha) Umeshaisikia hii?
    Kutoka kwa A.Y

    Chorus.
    (Yule) Nampenda sana jinsi alivyo (Yule)
    Nampenda sana jinsi alivyo simple.
    (Yule) Nampenda sana jinsi alivyo, nitafanyaje?
    PATAMU HAPO

    Verse I.
    Anavyotabasamu ndipo anaponipa hamu,
    Sura umbo lake basi lanipa wazimu,
    Nataka kumfuata, Nahisi atakataa,
    Naogopa akinimwaga, story zitazagaa.
    Napenda miondoko yake, tabia yake.
    Umaskini wangu utanifanya nisimpate.
    Yule , anayesumbua akili yangu.
    Yule, anayeumiza moyo wangu.
    Najua hafahamu, najua hafahamu,
    Moyoni mi nabaki na mawazo. Lakini

    Verse II.
    Tatizo hajui, Bila penzi lake maze sijitambui.
    Mi nitafanyeje, Hata nikimuona  mdomo unajaa mate
    (no x 6)
    Napomuonaa, pindi tukikutana. Iwe club, kapozi na rafiki zake.
    Ua tabu, napofikiria ni vipi nimfuate.
    Muda utafika napo ukweli ntamueleza.
    Nakosa raha pale washkaji wakinicheka…
    Sijitambui, nae hajui kama kwake nimefika…

    Chorus.
    (Yule) Nampenda sana jinsi alivyo (Yule)
    Nampenda sana jinsi alivyo simple.
    (Yule) Nampenda sana jinsi alivyo, nitafanyaje?
    PATAMU HAPO

    Bridge.
    Anavutia/cha ajabu hajidai.
    Nataka awe wangu tu, lakini kumwambia ndo siwezi.

    Chorus.
    (Yule) Nampenda sana jinsi alivyo (Yule)
    Nampenda sana jinsi alivyo simple.
    (Yule) Nampenda sana jinsi alivyo, nitafanyaje?
    PATAMU HAPO

    Written by: Ambwene Yessayah.
    Produced by: Steve Jean.
    Video by: Paparazzi Production.


    Usijaribu

    Intro: Let me talk to ya! Nataka kusema sana (No si sana) kuhusu watu wa aina
    fulani, mzeiya A.Y sema

    Chorus.
    Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba x 4
    Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao x 4

    Verse I.
    Yatazame vyema macho yangu right now,
    Nishapitia mambo mengi hata zaidi yao.
    Unapong’ata kwangu na kupulizia kwao,
    Unapochoka zaidi baada ya kuona mi nacheka nao.
    (Oh) Leo nakupa ukweli baada ya kuona unanispy,
    Cheza nami mbali sitaki hata unisabahi.
    (Sikujui) Niaje nipoteze muda nikuchunguze,
    (Hunijui) Vipi utunge uzushi kwangu uyasambaze.
    Mind your business hujui style ya Maisha yangu,
    Basi sitaki ubishe hadi kwenye anga zangu.
    Kila siku unayafuatilia, nayoyahangaikia,
    Lakini huwezi kuniharibia.
    Usione nimeshhh ukataka kupima,
    Nilikuona mwema kumbe zzzz nishakusoma.
    Nikiwepo mtu poa, nikiondoka unanichoma,
    Sasa unapochoma kama unaoga nje mchana ah.
    Niko imara zaidi ya chuma cha pua,
    Sitabiriki ujio wangu moyo wako unajua.
    Mlango wa ngome yangu mjomba noma ngumu kuingia,
    Ndo maana bado mi nakamua border nyingi napasua.

    Bridge.
    Shida zangu kwani zinakuhusu nini (wewe)
    Hata raha zangu zinakuhusu nini (wewe)
    Pia Maisha yangu yanakuhusu nini (wewe)
    OYAA X 2  (OYAA X 2)

    Chorus.
    Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba x 4
    Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao x 4

    Verse II.
    Usione watu wamechill wametulia, Busy
    Basi ukaona easy kuwachezea, ukidhi.
    Kupandikiza chuki news kudandia,
    Please, sitaki lawama kama vipi we potea
    Fanya usepe tu kwangu, kwangu hupati kitu fool
    Niogope kama OGOPA full wa mbuzi kama FID Q
    (A.Y x2) Bado nafanya mema huh
    Nikipata, nikikosa namshukuru Mungu tu,
    Kikulacho mbona kinguoni mwako.
    Wanaokuua mbona wa karibu yako,
    We unashangaa nani anauza file lako.
    Kama Adili kama mi (Bora niwe peke yangu).
    Deal zako ka zinabuma basi hasira usilete kwangu.
    Kama zali oh si lako jitume kibingwa wangu.
    Sio unakaa tu, kazi tu, kupiga majungu.
    Napo muda unapata bado unapiga virungu.
    Mchawi hana alama wapo (humuhumu).
    Asiyependa uendelee ni (mchawi tu).
    Hakosi uja kwako hodi kila saa (Ngo,ngo)
    Ndani chuki nje kila saa anakupa tano. (Ngum, Ngum).

    Bridge.
    Shida zangu kwani zinakuhusu nini (wewe)
    Hata raha zangu zinakuhusu nini (wewe)
    Pia Maisha yangu yanakuhusu nini (wewe)
    OYAA X 2  (OYAA X 2)

    Chorus.
    Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba x 4
    Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao x 4

    Bridge
    (Aaah) Usijaribu kuchunguza sura hii
    (Aaah) Kama ina raha ama zzzz
    (Aaah) Usilete tabia za kizamani.
    Maisha yangu yanakuhusu nini

    Outro.
    Au vipi bwana , Ni hayo.
    Huu ni muda na kila mtu kujiheshimu rafiki yangu.
    Haijalishi wewe ni nani na unatoka wapi.
    Niachie mimi nifanye kama mimi.
    Sababu siwezi kufanya kama wewe na wewe huwezi kufanya kama mimi.
    Sikiliza Ambwene, hili ni bonge la dude, bonge la beat kutoka kwa OGOPA.
    Matrack kama haya yanatakiwa kusikilizwa mtaani. Chuki kibao zipo, kwa nini?
    USICHUKULIE POA X 2

    Written by: Ambwene Yessayah & Fid Q
    Produced by: Ogopa Deejays
    Video by: Ogopa video.

 
©2007 AY entertainment • Privacy Policy        home | myspace | useful links
contact me