| |
Binadamu
Intro: This is A.Y from Tanzania, Maurice Kirya and Hamdee from Uganda.
It’s a dedication to all African who living in poverty.
Verse I.
Usiombee mambo yaharibike.
Pesa usiishike, mfano wa mti upukutike.
Utaonekana si lolote si chochote.
Utaonekana karaha kwa watu siku zote.
Walimwengu hawatakupa mikono.
Magonjwa yatakuvuta ndani ya shimo.
Utakata tamaa, utaandama na balaa.
Pumzi hutovuta kwa raha, kweli usiombee kuwahi.
Survive for fittest; never trust nobody in this world of weakness
Watakukana hata kama ndugu zako.
Watadiriki sema hawajui hutokako
Mama acha kulia, Hayo uliyonayo ni majaribu tu ya dunia. Ipo siku mambo yako yatatulia.
Utasahau hata Mabaya ya zamani uliyopitia ooh hii dunia…
Chorus.
Bagalalinaa, Gendo kole,
You should think about tomorrow
Not only today
Bagalalinaa, Gendokolee
Uuh, Gendokoleee
Yeeeh
Verse II.
Wapo wapi marafiki uliokuwa nao
Enzi zile pesa imekutembelea
Wako wapi sasa? Hawapo wamekukimbia
Sasa huko waliko tayari wanakukandia.
Ada ya watoto hujalipia, kodi ya chumba nayo unadaiwa,
unazidi changanyikiwa. Hata unajuta oh kwanini ulizaliwa.
Piga moyo konde, Maisha uyashinde.
Bado safari ndefu yenye miba na mabonde
Usiweke kinyongo hata kama walikutupa
Remain strong in this world.
Don’t be jealous, Dat’s all…
Chorus.
Bagalalinaa, Gendo kole,
You should think about tomorrow
Not only today
Bagalalinaa, Gendokolee
Uuh, Gendokoleee
Yeeeh
Bridge
Binadamu sio watu.
Ukiwa na shida hutowaona.
Ona sasa wamekimbia.
Ona sasa wamekimbia.
Chorus.
Written by: - Ambwene Yessaya, Hamdee Kiwamba & Maurice kirya
Produced by: - Henry from No End Production.
Mixed by: - Master Jay from MJ Production
Video by: - Paparazzi.
|
Yule
Intro: (Aha) (Aha) Umeshaisikia hii?
Kutoka kwa A.Y
Chorus.
(Yule) Nampenda sana jinsi alivyo (Yule)
Nampenda sana jinsi alivyo simple.
(Yule) Nampenda sana jinsi alivyo, nitafanyaje?
PATAMU HAPO
Verse I.
Anavyotabasamu ndipo anaponipa hamu,
Sura umbo lake basi lanipa wazimu,
Nataka kumfuata, Nahisi atakataa,
Naogopa akinimwaga, story zitazagaa.
Napenda miondoko yake, tabia yake.
Umaskini wangu utanifanya nisimpate.
Yule , anayesumbua akili yangu.
Yule, anayeumiza moyo wangu.
Najua hafahamu, najua hafahamu,
Moyoni mi nabaki na mawazo. Lakini
Verse II.
Tatizo hajui, Bila penzi lake maze sijitambui.
Mi nitafanyeje, Hata nikimuona mdomo unajaa mate
(no x 6)
Napomuonaa, pindi tukikutana. Iwe club, kapozi na rafiki zake.
Ua tabu, napofikiria ni vipi nimfuate.
Muda utafika napo ukweli ntamueleza.
Nakosa raha pale washkaji wakinicheka…
Sijitambui, nae hajui kama kwake nimefika…
Chorus.
(Yule) Nampenda sana jinsi alivyo (Yule)
Nampenda sana jinsi alivyo simple.
(Yule) Nampenda sana jinsi alivyo, nitafanyaje?
PATAMU HAPO
Bridge.
Anavutia/cha ajabu hajidai.
Nataka awe wangu tu, lakini kumwambia ndo siwezi.
Chorus.
(Yule) Nampenda sana jinsi alivyo (Yule)
Nampenda sana jinsi alivyo simple.
(Yule) Nampenda sana jinsi alivyo, nitafanyaje?
PATAMU HAPO
Written by: Ambwene Yessayah.
Produced by: Steve Jean.
Video by: Paparazzi Production.
|
Usijaribu
Intro: Let me talk to ya! Nataka kusema sana (No si sana) kuhusu watu wa aina
fulani, mzeiya A.Y sema
Chorus.
Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba x 4
Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao x 4
Verse I.
Yatazame vyema macho yangu right now,
Nishapitia mambo mengi hata zaidi yao.
Unapong’ata kwangu na kupulizia kwao,
Unapochoka zaidi baada ya kuona mi nacheka nao.
(Oh) Leo nakupa ukweli baada ya kuona unanispy,
Cheza nami mbali sitaki hata unisabahi.
(Sikujui) Niaje nipoteze muda nikuchunguze,
(Hunijui) Vipi utunge uzushi kwangu uyasambaze.
Mind your business hujui style ya Maisha yangu,
Basi sitaki ubishe hadi kwenye anga zangu.
Kila siku unayafuatilia, nayoyahangaikia,
Lakini huwezi kuniharibia.
Usione nimeshhh ukataka kupima,
Nilikuona mwema kumbe zzzz nishakusoma.
Nikiwepo mtu poa, nikiondoka unanichoma,
Sasa unapochoma kama unaoga nje mchana ah.
Niko imara zaidi ya chuma cha pua,
Sitabiriki ujio wangu moyo wako unajua.
Mlango wa ngome yangu mjomba noma ngumu kuingia,
Ndo maana bado mi nakamua border nyingi napasua.
Bridge.
Shida zangu kwani zinakuhusu nini (wewe)
Hata raha zangu zinakuhusu nini (wewe)
Pia Maisha yangu yanakuhusu nini (wewe)
OYAA X 2 (OYAA X 2)
Chorus.
Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba x 4
Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao x 4
Verse II.
Usione watu wamechill wametulia, Busy
Basi ukaona easy kuwachezea, ukidhi.
Kupandikiza chuki news kudandia,
Please, sitaki lawama kama vipi we potea
Fanya usepe tu kwangu, kwangu hupati kitu fool
Niogope kama OGOPA full wa mbuzi kama FID Q
(A.Y x2) Bado nafanya mema huh
Nikipata, nikikosa namshukuru Mungu tu,
Kikulacho mbona kinguoni mwako.
Wanaokuua mbona wa karibu yako,
We unashangaa nani anauza file lako.
Kama Adili kama mi (Bora niwe peke yangu).
Deal zako ka zinabuma basi hasira usilete kwangu.
Kama zali oh si lako jitume kibingwa wangu.
Sio unakaa tu, kazi tu, kupiga majungu.
Napo muda unapata bado unapiga virungu.
Mchawi hana alama wapo (humuhumu).
Asiyependa uendelee ni (mchawi tu).
Hakosi uja kwako hodi kila saa (Ngo,ngo)
Ndani chuki nje kila saa anakupa tano. (Ngum, Ngum).
Bridge.
Shida zangu kwani zinakuhusu nini (wewe)
Hata raha zangu zinakuhusu nini (wewe)
Pia Maisha yangu yanakuhusu nini (wewe)
OYAA X 2 (OYAA X 2)
Chorus.
Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba x 4
Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao x 4
Bridge
(Aaah) Usijaribu kuchunguza sura hii
(Aaah) Kama ina raha ama zzzz
(Aaah) Usilete tabia za kizamani.
Maisha yangu yanakuhusu nini
Outro.
Au vipi bwana , Ni hayo.
Huu ni muda na kila mtu kujiheshimu rafiki yangu.
Haijalishi wewe ni nani na unatoka wapi.
Niachie mimi nifanye kama mimi.
Sababu siwezi kufanya kama wewe na wewe huwezi kufanya kama mimi.
Sikiliza Ambwene, hili ni bonge la dude, bonge la beat kutoka kwa OGOPA.
Matrack kama haya yanatakiwa kusikilizwa mtaani. Chuki kibao zipo, kwa nini?
USICHUKULIE POA X 2
Written by: Ambwene Yessayah & Fid Q
Produced by: Ogopa Deejays
Video by: Ogopa video.
|
|
|
|
|